HAWA NDIYO MABABU WA MOJA KWA MOJA WA BINADAMU


Kuna kipindi katika historia ya mabadiliko ya mwanadamu ambayo wanasayansi bado hawayaelewi vizuri.

Ni kidogo kinachojulikana kuhusu enzi hizi, ambazo zinajulikana kuwa mkanganyiko , kwasababu wataalamu bado hawakubaliani kuhusu spishi ya binadamu aliyekuwepo na kwamba wanawakilisha enzi zisizojulikana kati ya Homo erectus na binadamu wa sasa.

Na sasa kundi moja la watafiti limetaja spishi mpya ambayo inaweza kuangaza kuhusu mkanganyiko, huo ambao kulingana na uchanganuzi wao, ndio mababu wa moja kwa moja wa binadamu.

Ni kuhusu Homo bodoensis , ambao waliishi barani Afrika miaka 500,000 iliopita na ambao kulingana na wanzilishi wa utafiti huo , wanasaidia kukamilisha fumbo kuhusu wakati muhimu katika mabadiliko ya binadamu.

Lebo mpya

"Mkanganyiko huo unahusiana na enzi za Middle Pleistocene, muda unaojulikana kama Chibanian tangu 2020 , na ambao ulitokea kati ya miaka 774,000 na 129,000 iliopita.

Watalaamu hatahivyo hawaelewi mabaki yanatoka kutoka kwa spishi katika kipindi hicho. Na haijulikani ni spishi ipi ilizaa nyengine.

Kipindi cha Chibanian ni muhimu kwa sababu huo ndio wakati Homosapiens waliibuka Afrika na Neanderthals huko Uropa.

Tatizo ni kwamba mabaki ya wakati huo ambayo yalitangulia Homo sapiens na Neanderthals, "hayajaelezewa vizuri na yanaeleweka kwa njia tofauti," kulingana na waandishi wa utafiti huo.

Kwa hili, watafiti wanamaanisha kuwa mabaki yaliopo kutoka enzi za Chibanian yamepewa jina kama Homo heidelbergensis au Homo rhodesiensis , aina mbili ambazo, kulingana nao, mara nyingi zimeelezewa kukinzana.


Via BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments