WATANO WAFARIKI KATIKA SHAMBULIZI LA MTU ALIYEJIHAMI KWA MISHALE NORWAY


Nchini Norway, mtu aliyekuwa amejihami kwa mishale amewashambulia na kuwauwa watu watano na kuwajeruhi wengine wawili katika mji wa Kongsberg, Kusini Magharibi mwa nchi hiyo. Mmoja wa waliojeruhiwa ni afisa wa polisi.

Polisi wanasema, mshukiwa,  mwenye umri wa miaka  37, amekamatwa, lakini lengo la shambulizi hilo halijabainika.

Ripoti zaidi zinasema, mshukiwa huyo alikuwa anatembea kwenye mji wa Kongsberg, akiwashambulia watu.

Mshambuliaji anasemekana kufanya tukio hilo ndani ya duka la jumla la Coop Extra iliopo upande wa Kongsberg magharibu.

Polisi wanaamini alitekeleza shambulio hilo peke yake, na watachunguza ikiwa ni kitendo cha ugaidi.

-RFI



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments