DULLA MBABE ACHAKAZWA TENA DAR NA BONDIA KUTOKA KONGO



BONDIA Abdallah Shaaban Pazi ‘Dullah Mbabe’ jana aliwasononesha Watanzania baada ya kuchapwa kwa pointi na Tshimanga Katompa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika pambano la raundi 10 ukumbi wa PTA, Temeke Jijini Dar es Salaam.

Dullah ambaye Agosti 20 alishindwa pia kwa pointi na Mtanzania mwenzake, Twaha Kassim ‘Kiduku’ – hakuwa katika ubora wake kabisa jana baada ya kuangushwa mara tatu ndani ya raundi ya saba, kabla ya kumalizia raundi tatu za mwisho na kuepuka kipigo cha Knockout.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments