Tanzia : MKE WA MZEE AUGUSTINE MREMA AFARIKI DUNIA


Mke wa Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema, mama Rose Mrema amefariki dunia.

Taarifa kutoka kwa mume wa marehemu Mzee Augustine Mrema zimeeleza kuwa amefariki dunia Alhamisi Septemba 16, 2021 majira ya saa 8 mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

“Nasikitika kutangaza kifo cha mke wangu (ROSE MREMA) kilichotokea jana tarehe 16/9/2021 saa 8 mchana Muhimbili kwa tatizo la shinikizo la damu,” Augustino Lyatonga Mrema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments