Pingamizi la Mbowe lagonga mwamba

Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi,imetupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu la kutaka kesi inayowakabili isisikilizwe na mahakama hiyo kwakuwa haina mamlaka ya kusikiliza kesi zenye mashtaka ya ugaidi.

Uamuzi huo umetolewa leo, Septemba Mosi, 2020 na Jaji Elinaza Luvanda ambaye baada ya kupitia hoja za pande zote mbili amesema Mahakama yake ina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya ugaidi na kwamba pingamizi lililowasilishwa na upande wa utetezi halina mashiko na hakubaliani nalo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments