Tanzia : WAZIRI WA ZAMANI BASILI MRAMBA AFARIKI DUNIA


ALIYEWAHI kuwa Waziri wa Fedha wa Tanzania, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo Jumanne, Agosti 17, 2021 katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam wakati akipatiwa matibabu.

Mramba aliwahi kuwa Waziri wa Fedha katika utawala wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambapo aliiongoza Wizara hiyo mwaka 2001-2005, baadaye Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko mwaka 2006 hadi 2008.

Familia ya Mramba imethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kueleza kuwa ni wanafamilia wachache wataruhusiwa kufika kutoa pole nyumbani kwa marehemu, Mawenzi Road, Oysterbay jijini Dar.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments