PROF. LUGHANO KUSILUKA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA VETERINARI TANZANIA

Profesa Lughano Kusiluka Mwenyekiti Mpya Baraza la Veterinari Tanzania.


Na Mwandishi Wetu 


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amemteua Profesa. Lughano Kusiluka kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Veterinari Tanzania.

Profesa Kusiluka ambaye ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe anachukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na Profesa. Rudovick Kazwala ambaye muda wake umeisha.

Uteuzi huo utaanza rasmi kesho Septemba 1, 2021 kwa kipindi cha miaka minne (4).

 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments