MBUNGE WA CCM JIMBO LA KONDE SHEHA MPEMBA FAKI AJIUZULU


Kulia aliyekuwa Mbunge Mteule wa Chama cha Mapinduzi CCM wa Jimbo la Konde visiwani Zanzibar Sheha Mpemba Faki (Picha kutoka mtandaoni).

Mbunge Mteule wa Chama cha Mapinduzi CCM wa Jimbo la Konde visiwani Zanzibar Sheha Mpemba Faki amejiuzulu katika nafasi yake hiyo kutokana na changamoto za kifamilia.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Shaka Hamdu Shaka imethibitisha kupokea barua ya kujiuzulu ya mbunge huyo leo, Agosti 2, 2021 kwa masikitiko makubwa.

Amesema Chama hakina uwezo kumzuia kwani ni haki yake ya msingi kama ilivyo haki yake msingi kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya ubunge ndani ya chama.

Sheha Faki aliibuka mshindi katika uchaguzi mdogo uliofanyika katika jimbo la Konde baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Khatib Said kufariki.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments