JAMAA ATIWA MBARONI KWA KUMDUNGA KISU MARA 17 MKEWE WALIYEACHANA



Mwanaume mmoja amekamatwa kwa kumdunga kisu mkewe waliyeachana mara 17 kulingana na simulizi ya mwanao na majirani waliofika eneo la tukio.

  Mtoto huyo alitoa maelezo muhimu kwa polisi amnbayo huenda yanaweza kusaidia kutatua kitendawili cha mauaji ya Esther Nyaga, muuguzi katika Zahanati ya Muruka Kandara, Kaunti ya Murang'a nchini Kenya.

 Iliripotiwa kuwa wapenzi hao walikuwa katika harakati za kutalikiana na Evans Njacha Kamau alikuwa ameamriwa na mahakama kutozuru boma lao.

Kulingana na familia, Esther alikuwa ameripoti kushambuliwa mara kwa mara na mumewe ambaye walikuwa wametengana lakini polisi walimpuuza tu.

 Kamau na Esther walioana mnamo 2010 lakini walitengana mnamo 2019. Wana watoto watatu (binti wa miaka 11 na wana wa kiume wa miaka 7 na 2).

Siku ya mauaji yake ya kikatili, jamaa zake walidai kwamba mtuhumiwa aliingia nyumbani na kuzima umeme.

 Mjakazi alimwona mtu aliyekuwa amejihami kwa kisu na bastola naye akaanza kukimbilia usalama wake akipiga mayowe. 

Esther alielekea jikoni baada ya kusikia vurugu kabla ya mshambuliaji kumtokea ghafla na kumuamuru kumpa pesa kabla ya kumuamuru kuelekea naye katika chumba cha kulala. 

Walipofika katika chumba chake cha kulala, mshukiwa alianza kumdunga kisu. 

Mshukiwa huyo aliondoka chumbani humo kumtafuta mjakazi ambaye alikuwa amejificha na ndiposa wakati huo watoto waliitambua sauti yake. 

Baadaye mshukiwa alihepa. Esther aliwaita watoto wake na kuwaambia wamjulishe jirani yao ili aje ampeleke hospitalini.

 Wakiwa njiani, Esther aliwaambia kuwa mumewe ndiye mshukiwa mkuu aliyemshambulia. 

Ripoti ya uchunguzi wa baada ya kifo ilionyesha kuwa muuguzi huyo alikuwa na majeraha mabaya tumboni na mshukiwa pia alijaribu kumchinja. 

Uchunguzi wa mauaji hayo bado unaendelea na mtuhumiwa atarudishwa kortini Jumatano, Agosti 18,2021.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments