RAIS WA AFGHANISTAN AKIMBIA NCHI YAKE


Rais Ashraf Ghani ameondoka nchini kwake, taarifa zinasema zimenukuu maofisa wa Afghanistan.

Taarifa ya kuondoka kwake imekuja mara baada ya Taliban ilivyofikia katika pembezoni mwa Kabul.

Makamu wa rais Amrullah Saleh naye aripotiwa kuondoka.

Taarifa za Bwana Ghani kuondoka zimekuja wakati ambao kumekuwa na mvutano mkubwa wa miji yote mikuu ya Afghanistan kudhibitiwa na wanamgambo wa Taliban.

Ofisi ya rais imeiambia Reuters kuwa "hawawezi kusema lolote kuhusu kuondoka kwa rais Ashraf Ghani kwasababu za kiusalama".
Wakati huohuo msemaji wa Taliban ameiambia BBC "hakutakuwa na visasi kwa watu wa Afghanistan.

Suhail Shaheen amewaakikishia wananchi kuwa ;"Tunawahakikishia raia wa Afghanistan, haswa wa mji wa Kabul, kuwa mali zao na maisha yao yatakuwa salama - hakuna atakayelipa kisasi kwa yeyote.

"sisi ni watumishi wa watu wa taifa hili."

Raia wengi wa Afghans wanahofia kurejea kwa ukatili uliofanyika mwaka 1990, ambapo watu waliuawa, walipigwa mawe na wasichana walipigwa marufuku kwenda shule.
Wanamgambo wa Taliban wamekaribia kuithibiti nchi nzima ya Afghanistan, huku mji mkuu wa nchi hiyo Kabul ukiwa umedhibitiwa pia na serikali.

Mapema leo Jumapili wanamgambo hao wameinyakua Jalalabad, bila mapigano. Jiji hilo lipo Mashariki mwa nchi.

Hatua hiyo ilifuatia kudhibitiwa kwa kwa mji muhimu wa shughuli za kiseriali wa Mazar-i-Sharif uliopo kaskazini hapo jana Jumamosi.

Kuzidiwa haraka kwa vikosi vya majeshi ya serikali kumemuweka Rais Ashraf Ghani katika shinikizo kubwa la kujiuzulu.

Rais Ghani anaonekana yupo njia panda katika kuamua la kufanya kati ya kujisalimisha au kuendeleza mapambano ya kudhibiti makao makuu ya nchi, Kabul.

Via BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments