TANZANIA U-23 MABINGWA CECAFA 2021



Timu ya Taifa ya Tanzania imtwaa Ubingwa wa Michuano ya Kombe la Chalenji ya Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) kwa vijana chini ya umri wa miaka 23 kwa mwaka 2021.

Tanzania ilikuwa ikipepetana na Burundi ambapo matokeo yalikuwa suluhu ya bilabial katika dakika 90 hivyo kwenda kwenye matuta ya penalty ndipo Tanzania ikabuka na ushindi wa penalti 6 kwa 5 za Burundi.

Mara ya mwisho Tanzania kuchukua kombe hilo ni mwaka 2010 huku Burundi ikiwa haijawahi kuchukua zaidi ya kuishia nafasi ya pili mwaka 2013.

Timu tisa zilishiriki michuano hiyo ambazo ni Tanzania, Burundi, Kenya, Uganda, Ethiopia, Eritrea, DR Congo, Sudan Kusini na Djibouti zilizogawanywa kwenye makundi matatu yenye timu tatu tatu kila moja.

Stori na Sifael Paul


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments