MBUNGE NEEMA LUGANGIRA ATOA NENO FEDHA ZINAZOKUJA NCHINI KWA AJILI YA NGOs

 

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM (NGOs Tanzania Bara) Neema Lugangira akizungumza  wakati wa  Uzinduzi wa Wiki ya Azaki imefanyika Jijini Dar es Salaam Julai 29 Julai 2021

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM (NGOs Tanzania Bara) Neema Lugangira amesema wakati umefika kuhakikisha fedha za ufadhili ambazo zinatoka nje ya nchi zinazokuja nchini ziweze kufanyiwa kazi na kutelezwa na NGOs na CSOs kutoka ndani ya nchi.

Aliyasema hayo Siku ya Uzinduzi wa Wiki ya Azaki imefanyika Jijini Dar es Salaam Julai 29 Julai 2021 ambapo alisema takwimu zinaonyesha kwamba zile fedha ambazo zinazoingia kwa ajili ya Sekta ya Azaki ni asilimia 1 pekee yake ndio zinaekwenda kwa CSOs, NGOs ambazo zimeanzishwa na Watanzania.

Mbunge Lugangira alisema kwa sababu takwimu zinaonyesha asilimia 99 ya fedha zinazotoka nje zinapita kupitia mashirika ambazo sio ya kiserikali lakini ni ya Kimataifa 
 
Alisema  ili miradi iwe endelevu lazima NGOs/CSOs za ndani ziweze kushiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo na ndio maana mara nyingi wanaona kuna miradi fulani ukishaasha ufadhili na mfadhili akishaondoka mradi unakuwa hauendelei.

Alisema pia mara nyingi Sekta ya Azaki wanahesabiwa kama sehemu ya Sekta Binafsi lakini Sekta Binafsi ni tofauti zaidi kwa sababu wale ni wafanyabiashara zaidi na wanapokwenda kuongea mwakilisha Sekta Binafasi hawezi kuwakilisha Sekta ya Azaki.

“Nimejaribu kutoa changamoto kama wadau mnatambulika kama sekta inayosimama inachangia kwenye maendeleo ili kufanya hivyo lazima waonyeshe mchango wao dhahiri ni upi ili waweze kutambulika”Alisema

Hivyo alisema ni matarajio yake itapoandaliwa wiki ya Azaki mwezi Octoba mwaka huu basi watapata majawabu kwenye eneo hilo na watafanya mikakati madhubiti ya kutoka asilimia 1 na iongezeke



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments