MWANZA FRIENDS WAKUTANA SHINYANGA MJINI KUZINDUA KATIBA ,KUSAKA FURSA ZA UWEKEZAJI


Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba na Nyaraka mbalimbali za Kikundi cha Mwanza Friends Association.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wanachama wa Kikundi cha Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma  Marafiki kutoka Mwanza maarufu ‘Mwanza Friends Association’ wanaofanya shughuli zao kwenye mikoa mbalimbali nchini Tanzania wamekutana Mjini Shinyanga kwa ajili ya kikao na kuzindua rasmi Katiba yao pamoja na kutafuta fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Shinyanga.

Wanachama hao wa Mwanza Friends Association wamefanya kikao chao kilichoambatana na ziara ‘Tour’ mkoani Shinyanga leo Jumamosi Julai 31 katika Hoteli ya Liga Mjini Shinyanga.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph amesema walianzisha kikundi hicho mwaka 2014 kwa lengo ya kusaidiana katika shida na raha.

“Kikundi cha Marafiki kutoka Mwanza 'Mwanza Friends Association' chenye Makao yake Makuu Jijini Mwanza kinaundwa na Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma wanaotoka Mkoa wa Mwanza lakini sasa wanaishi kwenye mikoa mingine nchini”,amesema Joseph.

“Sisi tunajihusisha na masuala ya kusaidiana kijamii katika shida na raha. Hivi sasa tuna wanachama 35 na tuna miradi ukiwemo mradi wa VIP Bar iliyopo Maduka Tisa Ilemela Jijini Mwanza”,ameeleza.

Amesema wanachama wa Mwanza Friends Association kutoka mikoa mbalimbali nchini wameamua kufanya kikao chao Mjini Shinyanga na kuzindua rasmi Katiba yao ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutafuta fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Shinyanga.

Joseph ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).

ANGALIA PICHA HAPA
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba ya Kikundi cha Mwanza Friends Association wakati wa kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Kulia ni Mweka Hazina, Respicius Rwegoshora, kushoto ni Katibu, Omary Haji.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akiwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao

Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akipata chakula
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akipata chakula
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.


Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments