SERIKALI YA TANZANIA YATOA MWONGOZO WA UDHIBITI WA MAAMBUKIZI YA COVID - 19 KATIKA SHULE, VYUO NA TAASISI ZA ELIMU


Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Prof. Abel Makubi akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma leo wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 kwenye shule na Taasisi za Vyuo zinazotarajiwa kufunguliwa hapo kesho.

Mwongozo huu unalenga kuweka mazingira wezeshi katika maeneo ya Taasisi za elimu ikiwa ni pamoja na; Vyuo, shule za sekondari, shule za Msingi, shule za awali na vituo vya kulelea watoto wadogo mchana (Day care centres) kabla ya wanafunzi kurejea shule na vyuo na kuendelea na masomo katika kipindi hiki cha mlipuko wa Homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi aina ya Corona.

Katika kufanikisha uwepo wa mazingira hayo, Mwongozo umezingatia maeneo makuu manne ambayo ni Maandalizi ya mazingira na taasisi za elimu kabla ya kufunguliwa, Uchunguzi wa Afya, Usafiri wa kwenda na kurudi shule na vyuo na Mazingira ya kujifunzia.

Maandalizi ya Mazingira ya Taasisi za elimu kabla ya kufunguliwa,Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara zote zinazosimamia vyuo na taasisi za mafunzo wanashauriwa kuhakikisha mazingira salama ya shule, vyuo na Taasisi za elimu kabla wanafunzi kurejea ili kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19. Katika kuandaa mazingira.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments