RAIS SAMIA AMTEUA MSANII NIKK WA PILI KUWA DC KISARAWE, JOKATE APELEKWA TEMEKE, MWIGIZAJI CHOPA MCHOPANGA ALAMBA RORYA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Msanii Nickson Simon John maarufu Nikk wa Pili kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.

DC mteule Nikk wa Pili anachukua nafasi ya Jokate Mwegelo ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

Vilevile, Rais Samia amewateua baadhi ya waliokuwa wabunge lakini kwa sababu mbalimbali wakashindwa kurejea bungeni. Wateule hao ni Joshua Nassari (Bunda), Halima Bulembo (Muheza) na Peter Lijualikali (Nkasi).


Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mwigizaji Juma Chikoka maarufu Chopa Mchopanga kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara.

Pia Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Basilla Mwanukuzi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga, Basilla aliwahi kuwa Miss Tanzania 1998.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments