MHE.CHAMUHIRO ATEMBELEA BANDA LA BRELA KATIKA MAONESHO YA WADAU WA SEKTA YA UJENZI

 

Waziri wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Mhandisi Leonard Chamuhiro, akipatiwa maelezo na maafisa wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), alipotembelea banda hilo mapema leo, baada ya ufunguzi wa maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika leo na kesho katika viwanja vya Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Maafisa wa BRELA kutoka kushoto ni Afisa Usajili Bw. Englibert Barnabas, Msaidizi wa Usajili Bi. Yvonne Massele na Afisa Leseni Bi. Saada Kilabula.

Maafisa wa BRELA wakitoa elimu na huduma kwa watembeleaji wa Maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi yanayofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Afisa Leseni wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Saada Kilabula ( aliyesimama kushoto) akitoa maelekezo ya huduma zitolewazo na BRELA kwa Msanifu majengo Bw. E.Nnunduma, katika maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, tarehe 27 -28 Mei, 2021.

Afisa Usajili kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bw. Englibert Barnabas (kulia), akitoa ufafanuzi wa huduma zitolewazo na BRELA kwa mteja kutoka Kampuni ya Agrovision Limited Bw. Arfaan Ahmed Alwani, alipotembelea banda la BRELA, katika maonesho ya wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments