Picha : RAIS SAMIA AONGOZA WAFANYAKAZI MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2021 JIJINI MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Wafanyakazi mbalimbali katika Kilele cha Sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi Kitaifa ambazo zimefanyika Jijini Mwanza leo tarehe 01 Mei, 2021 katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwasili katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Kitaifa leo Mei 1, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Kitaifa leo Mei 1, 2021.
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa ukiwasili katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Kitaifa leo Mei 1, 2021.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza tayari kwa maadhimisho ya Mei Mosi.
Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki katika maadhimisho hayo wakiwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akiwasili uwanjani.
Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo akiwasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Yustino Ndugai akiwasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Isdory Mpango akiwasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. Philip Isdory Mpango akiteta na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassim Majaliwa.
Baadhi ya wafanyakazi wakimlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwasili.
Wafanyakazi wa Wizara mbalimbali, Mashirika ya Umma, Taasisi za Serikali pamoja na Sekta Binafsi wakiwa kwenye maandamano wakati wa sherehe za Mei Mosi, zinazofanyika katika Uwanja wa Kirumba, jijini Mwanza.









Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments