Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kimbunga Jobo kimepungua nguvu kwa haraka baada ya kuingia katika mazingira yenye mzunguko wa upepo kinzani.
Taarifa iliyotolewa na TMA leo Jumamosi Aprili 24, 2021 imeeleza kuwa kimbunga hicho kimekuwa hafifu na kinasafiri kwa kasi ya kilometa 18 kwa saa baharini tofauti na spidi ya kilometa 60 kwa saa iliyokuwa imetabiriwa awali.
TMA imesema kimbunga hicho kilichopo Bahari ya Hindi kwa sasa kipo umbali wa kilomita 200 mashariki mwa kisiwa cha Mafia.
“Kimbunga hafifu cha Jobo kinatarajiwa kusababisha vipindi vya mvua kubwa katika maeneo machache hususan ya ukanda wa Pwani kadri kinavyosogea nchi kavu kwa siku ya leo Aprili 24 na kesho Aprili 25, 2021,” inaeleza taarifa hiyo.
Maeneo yanayotarajiwa kupata athari za moja kwa moja ni pamoja na mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani ikiwemo kisiwa cha Mafia, Dar es Salaam pamoja na kisiwa cha Unguja.
Aidha TMA imetahadhalisha kuwa uwepo wa kimbunga hafifu baharini, unatarajiwa kusababisha mawimbi makubwa.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin