RAIS SAMIA AWASILI UGANDA, KUSHUHUDIA KUSAINIWA MKATA BOMBA LA MAFUTA


Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassana, amewasili nchini Uganda kwa ziara ya siku moja ambapo pamoja na mambo mengine atashuhudia utiwaji saini kati ya Serikali ya Uganda na kampuni tanzu ya uzalishaji Mafuta ya Afrika Mashariki (EACOP).

Alipowasili katika Ikulu ya Entebe Rais samia Suluhu Hassan, amepokewa na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Museven na kisha kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake na kikosi cha jeshi cha nchi hiyo.

Katika ziara hiyo Rais Samia Suluhu Hassana atakuwa na mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake Rais Museven kabla ya hafla ya kutiliana Saini baina ya EACOP na serikasli ya Uganda.

Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Chongoleani Jijini Tanga linatarajiwa kuanza kujengwa mara baada ya kukamilika kwa mikataba yote baina ya wadau wa wanaohusika na mradi huo.

Hii ni ziara ya kwanza kwa Rais Samia Suluhu Hassan nje ya nchi tangu aapishwe kuwa Rais wa Tanzania Machi 19,2021.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments