WANAWAKE WATATU WAKAMATWA KWA KUWALEWESHA NA KUWAIBIA WANAUME BAA




Polisi huko Nyeri, nchini Kenya wanawashikilia wanawake watatu wanaodaiwa kuibia wanaume katika kumbi za starehe.

Wanawake hao wanaojulikana kwa majina Rita Okuto, Caroline Kariuki na Caroline Wanjiku walikamatwa usiku wakiwa wanazunguka nje ya muda watu wanaoruhusiwa kuwa nje baada ya Kenya kuweka “Lockdown”.

Watuhumiwa walikutwa na simu sita, tablet, tarakilishi mpakato (laptop) pamoja na vitambulisho, kadi za ATM za watu wengine pamoja na dawa zinazosadikiwa kutumika katika kuwafanya wahanga wao kusinzia kabla ya kuwaibia.

Wanaume wawili walijitokeza kushitaki katika kituo cha polisi Njeri na kufanikiwa kupata simu zao na kusema kuwa walikuwa na wanawake hao baa.

Washitakiwa watafikishwa mahakamani Aprili 6, kwa ajili ya kusomewa mashitaka.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments