MWANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA MAMBA

Janeti Mganga (8) aliyekuwa anasoma darasa la kwanza shule ya msingi Busikimbili iliyoko kata ya Maisome, Halmashauri ya Buchosa, wilayani Sengerema mkoani Mwanza ameuawa na mamba wakati akioga kwenye Ziwa Victoria huku baadhi ya viungo vya mwili wake vikiwa vimenyofolewa na kutafunwa na mamba huyo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole, amesema mwanafunzi huyo alikutwa na tukio hilo wakati alipokua akioga na wanafunzi wenzake katika Ziwa Victoria.

Kipole amewasihi wazazi wasiwaruhusu watoto wao kwenda kuogelea ziwani badala yake wateke maji na kwenda majumbani.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments