RAIS MAGUFULI AITAKA WIZARA YA MADINI KUTOCHELEWESHA MRADI WA UZALISHAJI MADINI YA NIKELI
Tuesday, January 19, 2021
Rais Dkt John Magufuli amesema hatua ya kusainiwa kwa mradi wa uzalishaji madini ya Nikeli kati ya Serikali na kampuni ya LZ Nickel Limited, inaashiria kuwa sasa Tanzania itaanza kufaidi matunda ya kuwa na madini hayo hapa nchini.
Akihutubia baada ya kushuhudia utiaji saini mkataba wa mradi huo mjini Bukoba mkoani Kagera, Rais Magufuli amesema kuwa Watanzania wamechoka kusubiria mradi huo ambapo tangu mwaka 1976 madini hayo yaligundulika hapa nchini.
Rais Magufuli amesema, Tanzania ni tajiri kwenye sekta ya madini na hivyo ni wakati muafaka sasa kuanza kufaidi matunda ya utajiri huo kwa kutafuta Wawekezaji wenye nia nzuri na maendeleo ya Tanzania.
Akizungumzia mradi huo Rais Magufuli amesema, Madini hayo ya Nikeli yatasaidia ukuaji wa uchumi wa Tanzania hasa kipindi hiki ambacho nchi inatekeleza mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR).
Ameitaka wizara ya Madini kutochelewesha mradi huo na kutoa ushirikiano kwa Wawekezaji hao ili kuharakisha uzalishaji wa madini ya Nikeli yanayotarajiwa kuzalishwa kutoka kwenye mradi wa Kabanga uliopo mkoani Kagera.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin