JKT YASITISHA MAFUNZO YA KUJITOLEA MWAKA 2020/2021


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limesitisha kwa muda mafunzo ya kujitolea ya JKT kwa mwaka 2020/2021 yaliyokuwa yaanze hivi karibuni kwenye kambi mbalimbali nchini.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya JKT imeeleza kuwa mafunzo hayo yamesitishwa hadi hapo itakapotangazwa tena.

Kutokana na kusitishwa huko, JKT imewataka vijana wote ambao walichaguliwa na tayari wameripoti kwenye kambi walizopangwa, kurejea majumbani mwao.

Aidha, wale ambao walikuwa bado hawajaripoti kambini, wametakiwa kutoripoti.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments