TANESCO YAWAPANDISHA KIZIMBANI WATU SABA KWA KUINGILIA MIUNDOMBINU YA UMEME


Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) limewapandisha kizimbani watu sita katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Desemba 2, 2020 kwa tuhuma za kuingilia miundombinu ya umeme na kulisababishi Shirika hasara ya shilingi milioni sita.(6,000,000).

Watuhumiwa hao ni pamoja na Boniphace Emmanuel, Elitruda Ancelim, Twalib Ibrahim, Mwarami Omary, Vumilia Sultani Kaambi, James Joseph na Haidary Islamy.

Hata hivyo upande wa mashtaka umesema upelelezi bado unaendelea na haukuwa na kipingamizi katika kutolewa dhamana ambapo hakimu anayesikiliza kesi hiyo alisema kila mshtakiwa anapaswa kulipa shilingi milioni moja na kuwa na mdhamini mmoja baye sharti awe mtumishi wa Umma.

Kesi imehairishwa hadi tarehe 16.12.2020.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments