RAIS MAGUFULI : BORA WAZIRI UFANYE UAMUZI MBAYA KULIKO KUTOFANYA KABISA....AKEMEA KUVUJISHA SIRI ZA SERIKALI MTANDAONI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amewataka Mawaziri na Manaibu Mawaziri kwenda kuchapa kazi huku akiwasisitiza kufanya maamuzi yanayohusu maslahi ya nchi.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Jumatano Disemba 9,2020 Ikulu Chamwino Dodoma wakati akiwaapisha Mawaziri 21  na Manaibu Mawaziri 22 aliowateua Disemba 5,2020.

"Mkachape kazi kweli kweli. Nawaomba mawaziri na naibu mawaziri mkafanye maamuzi, ni nafuu ukafanye uamuzi mbaya kuliko kutokufanya uamuzi kwa sababu tatizo letu jingine tulilonalo unashindwa kutoa uamuzi kwa sababu hutaki kuonekana mbaya",amesema Rais Magufuli.

 Kafanyeni uamuzi hasa unaohusu maslahi ya taifa, uamuzi utakaosaidia kuondoa shida ya wanyonge waliopo vijijini na mimi naamini nimechagua watu wote watakaokwenda kufanya maamuzi",amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia amewataka watendaji wa serikali kutumia vizuri mitandao ya kijamii na kuepuka kutuma nyaraka za serikali kwenye magroup 'Whatsapp'.

“Ndani ya Serikali sasa hivi kuna ugonjwa mmoja hata mawasiliano yanatumwa kwenye group barua nyingine za siri, tunatakiwa tukutane saa flani mahali flani ajenda yetu ni hii unakuta labda ma-DAS wanaandikiana hivyo au ma- DC, Mawaziri au Makatibu Wakuu ndiyo maana siri ndani ya serikali zinavuja,” amesema Rais Magufuli.

"Fanyeni kazi kwa uadilifu na mkazingatie maadili. Hii teknolojia mpya mkaitumie vizuri,muache kutumia nyaraka za serikali kwenye magroup",amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments