WAZIRI MKUU WA UINGEREZA AJITENGA TENA BAADA YA KUKUTANA NA MTU MWENYE CORONA


 Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ametangaza kujitenga baada ya kukutana na Mbunge wa Ashfield, Lee Anderson ambaye baadaye alithibitishwa kuwa na Virusi vya Corona.

Johnson amesema, alitafutwa na Mamlaka na kutakiwa kufanya hivyo kama taratibu zinavyoelekeza, japokuwa hana dalili zozote za COVID19 baada ya kuwa karibu na Anderson kwa takriban dakika 35.

Mwezi Aprili, Waziri huyo aligundulika na Ugonjwa huo na kulazwa ICU kwa siku 3. Hadi sasa Uingereza imerekodi visa 1,369,318 na vifo 51,934.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments