WATATU KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUCHOMA MOTO MABWENI YA SHULE KILIMANJARO


Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imewafikisha mahakamani washtakiwa watatu wanaohusishwa na matukio ya kuchoma moto bweni la Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Uchira na bweni la Shule ya Sekondari Ebeneza Sango zilizopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, Mkurugenzi Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Oswald Tibabyekomya amesema katika tukio la kuchoma moto bweni la shule ya Sekondari ya  Wasichana  Uchira yupo mwalimu mmoja pamoja na mwanafunzi mmoja.

Ameeleza kuwa katika tukio la kuchoma moto bweni la Shule ya sekondari Ebeneza wamemfikisha mahakama mwanafunzi mmoja.

Aidha, amefafanua kuwa, kulingana na upelelezi uliofanyika wamebaini kichocheo kikubwa ni mahusiano mabaya na ushawishi wa vikundi rika visivyofaa shuleni.

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imesema upelelezi wa matukio hayo pamoja na mengine yanayofanana na haya bado yanaendelea. 

 

Credit:TBC



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments