WALIMU WAWILI KORTINI TUHUMA ZA MAUAJI YA MWANAFUNZI
Saturday, November 07, 2020
Walimu wawili wa Shule ya Awali na Msingi ya Holly Cross Nursery iliyopo Temeke jijijini Dar es Salaam wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na shtaka la kudaiwa kumuua mwanafunzi wa Shule hiyo, Cathbert Chawe.
Washtakiwa hao ni, Leahdorice Agunda(35) na Maths Laizer ambaye ni Mkazi wa Mtoni Kijichi.
Wakisomewa hati ya mashtaka na Wakili wa Serikali Mwandamizi,Wankyo Simon mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Yusto Ruboroga amedai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na shtaka moja ambao mnamo Septemba 14, 2020 katika shule ya awali na Msingi ya Holly Cross Nursery iliyopo maeneo ya Kijichi Wilaya ya Temeke wote Kwa pamoja wanadaiwa kumuua mwanafunzi wa shule hiyo, Cathbert Chawe huku wakijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Wankyo amedai kuwa upelelezi wa shauri Hilo bado haujakamilika na hivyo aliiomba mahakama hiyo ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Baada ya maelezo hayo Hakimu Ruboroga amesema washtakiwa hao hawarihusiwi kujibu chochote kwa kuwa kesi hiyo ni ya mauaji hivyo ameahirisha shauri hilo Hadi Novemba 19, mwaka huu.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin