BILIONI 66.8 KUTUMIKA UJENZI WA BARABARA YA TANGA HADI PANGANI

Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) Mkoa wa Tanga Mhandisi Alfred Ndumbaro akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani.


UJENZI wa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga hadi Pangani yenye urefu wa kilomita 50 unatarajiwa kutumia bilioni 66.8 na utamalizika kwa kipindi cha miaka miwili.

Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) Mkoa wa Tanga Mhandisi Alfred Ndumbaro alisema kwamba tayari mkandarasi alikwisha kupatikana wa kampuni kutoka nchini China ya Chicco na amekwisha kuripoti eneo la kazi.

Alisema mkandarasi huyo hivi sasa anaendelea na maandalizi ya kujenga kambi ya wahandisi ambao watasimamia mradi huo na wafanyakazi wake katika maeneo ya Tongoni na Geza.

“Kama Serikali ilivyohaidi kujenga kiwango cha lami Barabara ya Tanga hadi Pangani kilomita 50 na tayari mkandarasi amekwisha kupatikana na amekwisha ripoti eneo la kazi kampuni kutoka china inatiwa Chicco”Alisema Meneja huyo.

Meneja huyo alisema tayari mkandarasi huy ameanza kusafisha kilomita 14 ambazo hazina matatizo na fidia na yupo eneo la kazi anaendelea kufanya kazi wakati huo anaendelea kujenga kambi za wahandisi pale Tongoni huku akimalizia kambi nyengine Geza .

Alieleza pia baadhi ya mitambo inaendelea kuletwa huku akiwataka wananchi kwenye maeneo yote washirikiana mkandarasi kuweza kumsaidia ili asiibiwe vifaa au mafuta wakati akitekeleza majukumu yake.

“Ujenzi huu pia utatoa fursa za ajira kwa wakazi wa Tanga wakati mradi huo ukianza ajira madereva, vibarua na tumemwambia achukua wananchi wanaoishi kwenye maeneo ambapo mradi unatekelezwa”Alisema Meneja huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments