BIDEN APATA MAFANIKIO YATAKAYOMWEZESHA KUSHINDA KITI CHA RAIS WA MAREKANI


Mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha Democratic nchini Marekani, Joe Biden amepiga hatua muhimu kuelekea kupata ushindi baada ya kunyakua majimbo tete ya Michigan na Wisconsin usiku wa kuamkia leo.

 Katika taarifa fupi aliyoitoa akiwa pamoja na mgombea mwenza Harris Kamala, Biden amesema hawezi kujitangazia ushindi lakini ana matumaini kuwa zoezi la kuhesabu kura litakapomalizika wataibuka kuwa washindi. 

Kwa kunyakua majimbo hayo mawili, Biden amefikisha kura 264 za Baraza maalumu la wajumbe wanaomchagua rais dhidi ya 214 za rais Doanld Trump anayewania muhula wa pili.

 Trump amezungumzia mafanikio hayo ya Biden kwa hasira na tayari amewasilisha ombi la kufungua shauri dhidi ya matokeo hayo ikiwa ni pamoja na kutaka kura kuhesabiwa tena na katika baadhi ya majimbo ametaka zoezi la kuhesabu kura kusitishwa.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments