MWENYEKITI WA MTAA ASIMULIA JINSI MJUKUU WAKE WA MIAKA 7 ALIVYOCHINJWA NA MAMA YAKE

Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Doreen Aloyce,TimesMajira, Online Dodoma

Mtoto wa miaka saba aitwaye Willy Wiliam mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Ihumwa ameuawa kwa kuchinjwa shingo na mtu anayedaiwa kuwa ni mama yake mzazi, Grace William (45) kisha kutokomea kusikojulikana.

Tukio hilo limetokea usiku wa manane kuamkia Septemba 30,2020 katika Mtaa wa Ihumwa, nje kidogo ya Jiji la Dodoma ambako mtoto alikuwa akiishi na mama huyo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Ihumwa ambaye pia ni baba mzazi wa Grace, William Ngilimunji, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kwamba aliyekufa ni mjukuu wake. Alidai wakati mauaji hayo yanafanyika mtoto alikuwa amelala.

Amedai kwamba aliyehusika na mauaji hayo ni mama wa mtoto huyo ambaye ana matatizo ya akili na kwamba alikuwa akihudhuria kliniki Hospitali ya Wagonjwa wa Akili Mirembe, mkoani hapa.

Ngilimunji amesema mtoto wake huyo (mama wa marehemu) hana mume na amekuwa akiishi Ihumwa. 

Via TimesMajira

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments