Picha : TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YAKUTANA NA WADAU WA UCHAGUZI SHINYANGA… ‘YAONYA UVUNJIVU WA AMANI KWA KISINGIZIO CHA UCHAGUZI’



Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga


Na Kadama Malunde- Malunde 1 blog
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Nchini Tanzania (NEC) imekutana na wadau wa Uchaguzi mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba Oktoba 28,2020.

Mkutano huo uliofanyika leo Ijumaa Oktoba 2,2020 Mjini Shinyanga umefunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa dini, Baraza la Wazee,wawakilishi wa watu wenye ulemavu,vijana,wanawake,asasi za kiraia na waandishi wa habari.

Akizungumza, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard alivikumbusha vyama vya siasa na wagombea kuzingatia maadili ya uchaguzi katika kampeni zao ikiwemo kuepuka lugha za kashfa,maneno ya uchochezi yanayotishia usalama na amani ya nchi.

“Tume inasisitiza vyama vya siasa na wagombea kuhakikisha wanaepuka kufanya kampeni zinazoashiria ubaguzi katika misingi ya jinsi,ulemavu,ukabila,udini,maumbile au rangi”,alisema Leonard.

Aidha alibainisha kuwa wakati tume inaendelea kuratibu na kusimamia na kuendesha uchaguzi kwa kutumia sheria za uchaguzi ni vyema vyama vya siasa,wagombea na wananchi waelewe kuwa sheria zingine za nchi hazijasimama hivyo wajihadhari na vitendo ama matamshi ambayo yanaweza kusababisha vurugu kwa kisingizio cha uchaguzi.

“Tume inawahakikishia kuwa itasimamia uchaguzi mkuu 2020 kwa kuzingatia Katiba,sheria,kanuni na taratibu zinazosimamia uendeshaji wa uchaguzi.Lengo ni kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru,wa wazi,haki na wa kuaminika kwa kuweka mazingira sawa ya ushindani kwa wagombea na vyama vyote vinavyoshiriki”,alisema Leonard.

Alitumia fursa hiyo kuwaomba wadau wa uchaguzi kufikisha ujumbe sahihi kuhusu uchaguzi kwa wananchi ili kila mwenye sifa ya kupiga kura ajitokeze na kadi yake kupiga kura katika kituo alichojiandikisha ili kutimiza haki yake ya msingi ya kikatiba.

“Pamoja na Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kuna jumla ya wapiga kura 29,188,347, tume imefanya maandalizi mengine muhimu kama vile marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge za mwaka 2020 na Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani za mwaka 2020”,alisema.

Alieleza kuwa Tume ya uchaguzi kwa kushirikiana na serikali na vyama vya siasa waliandaa Maadili ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020.

“Maandalizi mengine ni manunuzi ya vifaa na uchapishaji wa nyaraka mbalimbali zikiwemo Fomu,maelekezo kwa watendaji wa uchaguzi na maelekezo kwa vyama vya siasa na wagombea,miongozo ya elimu ya mpiga kura na mwongozo wa watazamaji wa uchaguzi”,aliongeza Leonard.

Alisema tayari Tume imekamilisha mafunzo ya watendaji wa uchaguzi wakiwemo waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi, maafisa uchaguzi wa halmashauri na maafisa Tehama na kwamba mafunzo yaliyobaki ni kwa watendaji wa vituo.

Leonard alisema jumla ya wagombea wa vyama vya siasa 15 wameteuliwa na Tume ya uchaguzi kugombea nafasi ya Urais na imetoa vibali vya kutoa elimu ya mpiga kura kwa asasi za kiraia 245 kwa Tanzania Bara na Asasi za kiraia 7 kwa Tanzania Zanzibar.

“Tume ya uchaguzi pia imeruhusu Watazamaji wa ndani na nje katika uchaguzi mkuu 2020 ambapo imetoa vibali kwa asasi za kiraia na taasisi 97 za ndani na vibali kwa makundi 16 ya watazamaji wa nje”,alisema Leonard.

“Ushirikishwaji mwingine wa wadau ni kupitia mawakala wa vyama vya siasa kwani siku ya uchaguzi vyama vya siasa vimepewa nafasi ya kuweka wakala katika kila kituo cha kupigia kura. Wakala atakuwepo kituoni kwa ajili ya kuangalia taratibu za uchaguzi zinavyoendeshwa kituoni na kama zinazingatia sheria,kanuni,taratibu na maelekezo ya tume. Lengo kubwa ikiwa ni kulinda maslahi ya chama na wagombea”,alifafanua Leonard.

Akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu 2020, Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa alisema tume imekamilisha uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura ambapo hivi sasa kuna jumla ya wapiga kura 29,188,347 ambapo wapiga kura 29,059,507 wapo Tanzania Bara na 128,840 wapo Tanzania Zanzibar.

Nuru alisema pia kuna jumla ya wapiga kura 566,352 walioandikishwa na ZEC ambao watashiriki kupiga kura ya kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kati ya wapiga kura 29,188,347 walioandikishwa, wanawake ni 14,691,743 ambao ni sawa na 50.33%, wanaume ni 14,496,604 ambao ni sawa na 49.67%. Vijana kati ya umri wa miaka 18-35 ni 15,650,998 (vijana wa kiume ni 7,804,845, wa kike 7,846,153). Aidha kuna jumla ya watu wenye ulemavu 13,211 na kati yao 2,223 wana ulemavu wa macho, 4,911 wana ulemavu wa mikono na 6,077 wana ulemavu wa aina nyingine”,alifafanua Nuru.

Aliongeza kuwa tume itatumia vituo vya kupigia kura 80,155 katika zoezi la kupiga kura Oktoba 28,2020, kati ya vituo hivyo Tanzania Bara itakuwa na vituo 79,670 na Tanzania Zanzibar itakuwa na vituo 485.Vile vile tume itatumia vituo 1,412 vya ZEC kwa upande wa Tanzania Zanzibar ambapo jumla ya watendaji 320,620 watasimamia na kuendesha zoezi la upigaji kura vituoni na kwamba kila kituo kitakuwa na wapiga kura wasiozidi 500.

Alisema idadi ya majimbo ya uchaguzi mkuu 2020 ni 264 ambapo Tanzania Bara ina majimbo 214 na Tanzania Zanzibar ina majimbo 50 na kata zitakazotumika katika uchaguzi mkuu 2020 ni 3,956.

 Katika hatua nyingine alisema kwa mara ya kwanza katika uchaguzi mkuu 2020 vyama vya siasa vimesimamisha wagombea wengi wa kiti cha Rais hali inayoashiria ukuaji wa demokrasia nchini Tanzania.

"Tume ya uchaguzi imeteua wagombea wa kiti cha Rais/Makamu wa Rais kutoka vyama 15 vya siasa kati ya vyama 19 vyenye usajili wa kudumu. Katika uteuzi huo wanawake wawili walijitokeza na kuteuliwa kugombea kiti cha Urais na wanawake watano walijitokeza na kuteuliwa kugombea nafasi ya Makamu wa Rais",alifafanua Nuru.

Kwa upande wao wadau wa uchaguzi walioshiriki mkutano huo waliipongeza tume ya taifa ya uchaguzi kwa kukutana nao huku wakieleza kukerwa na baadhi ya kauli zinazotolewa na baadhi ya wagombea kwenye mikutano ya kampeni na kuiomba tume ya taifa ya uchaguzi na serikali kuchukua hatua dhidi yao ili kulinda amani ya nchi.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Oktoba 2,2020 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna katika Manispaa ya Shinyanga. Wa kwanza kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili akifuatiwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi na Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga. Wa kwanza kulia ni Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet akifuatiwa na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Oktoba 2,2020 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga. Wa kwanza kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili akifuatiwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi na Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga. Wa kwanza kulia ni Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet akifuatiwa na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akisisitiza jambo kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga. Alisema wakati tume inaendelea kuratibu na kusimamia na kuendesha uchaguzi kwa kutumia sheria za uchaguzi ni vyema vyama vya siasa,wagombea na wananchi waelewe kuwa sheria zingine za nchi hazijasimama hivyo wajihadhari na vitendo ama matamshi ambayo yanaweza kusababisha vurugu kwa kisingizio cha uchaguzi.
Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu 2020  kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu 2020  kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu 2020  kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu 2020  kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga. kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Kushoto ni Katibu wa Chama cha Watu wenye Ualbino Mkoa wa Shinyanga, Lazaro Anael akitoa msaada wa lugha ya alama kwa watu wenye ulemavu wa kutosikia (Viziwi) waliohudhuria mkutano wa wadau wa Uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga,  Soud Suleiman Kategile akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la KKKT Shinyanga na Simiyu,Trafaina Nkya akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Katibu Mwenza wa Kamati ya Amani Mkoa wa Shinyanga, Khalfan Ally akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Padre Simon Maneno kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Askofu  Raphael Machimu ambaye ni Katibu wa Kamati ya Amani mkoa wa Shinyanga, akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mdau wa Uchaguzi, Japhet Bulugu kutoka Brotherhood group akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mwenyekiti wa Kamati ya Amani mkoa wa Shinyanga, Sheikh Balilusa Khamis akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mdau wa uchaguzi Jonathan Kifunda Manyama kutoa shirika la Thubutu Africa Initiatives akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mwandishi wa habari wa Channel Ten, John Mponeja akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mdau wa uchaguzi George Nyanda kutoka shirika la Rafiki SDO akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mdau wa uchaguzi, John Myola kutoka Shirika la AGAPE ACP akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya watu wenye ulemavu mkoa wa Shinyanga, Richard Mpongo akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi mkoa wa Shinyanga, Justine Shindai akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Kushoto ni Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakiwa kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Katibu wa Baraza la Wazee Mkoa wa Shinyanga, Anderson Lyimo akichangia hoja kwenye mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye mkutano  ulioandaliwa na Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kupeana taarifa mbalimbali za mchakato wa uchaguzi na kujadiliana namna bora ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa viongozi wa dini baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa Baraza la wazee mkoa wa Shinyanga baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa wanawake baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa vijana baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa watu wenye ulemavu baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa Asasi za kiraia baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa Waandishi wa Habari baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Baraka Leonard, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga George Bangili,Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shinyanga Mjini, Geofrey Mwangulumbi,Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Fabian Kamoga.,Afisa Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Reteti Molloimet  na Afisa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuru Riwa wakipiga picha ya pamoja na Wawakilishi wa Waandishi wa Habari baada ya kufunga mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoa wa Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527