NEC YAMTANGAZA DK. JOHN POMBE MAGUFULI KUWA MSHINDI URAIS TANZANIA


Dkt John Pombe Magufuli
Dkt. John Pombe Magufuli
***

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza Dkt.John Pombe Magufuli kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa Mshindi wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura 12,516,252, akifuatiwa na Tundu Lisu wa  CHADEMA mwenye kura  1,933,271 huku  Bernard Membe kutoka ACT-Wazalendo akiwa amepata kura 81,129.

Akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage amesema kuwa jumla ya waliojiandikisha ni 29,754,669, na kura halali zilizopigwa ni 14,830,195 huku kura 261,755 zikikataliwa.

”Tume inamtangaza Dkt. Magufuli kuwa Rais wa Tanzania amepata kura nyingi halali kuliko wagombea wengine wote na tunamtangaza Mama Samia Hassan Suluhu kuwa Makamu wa Rais wa Tanzana”,amesema Jaji Mstaafu Kaijage

Jaji Mstaafu Kaijage amesema kuwa Rais Mteule pamoja na makamu wake watakabidhiwa cheti cha ushindi siku ya Jumapili.

Magufuli ameshinda uchaguzi huo uliofanyika Oktoba 28, 2020 ukijumuisha madiwani na wabunge, ambapo jumla ya majimbo 264 yameshiriki uchaguzi huo  na Jumla ya vyama 15 vilishiriki uchaguzi ngazi ya Urais.

Mwenyekiti huyo wa Chama Cha Mapinduzi, anaingia katika awamu yake ya pili ya uongozi, baada ya awamu ya kwanza kuanza mwaka 2015 na kumalizika 2020 na sasa ataendelea kwa kipindi cha 2020 hadi 2025.
***
Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha ni 29,759,699

Wapiga kura waliojitokeza Kura - 15,910,950

Idadi ya kura halali 14,830,195

Idadi ya Kura zilizokataliwa 261,755

Kura Walizopata Wagombea

Dkt John Pombe Magufuli CCM
Kura - 12,516,252

Leopard Lucas Mahona NRA
Kura -8787

John Paul Shibuda ADA- TADEA
Kura - 33,086

Muttamwega Mgaywa SAU
Kura - 14,922

Cecilia Augustino Mmanga (Demokrasia Makini)
Kura - 14,556

Maganja Yeremia Kurwa (NCCR)
Kura - 19,969

Lipumba Ibrahim Haruna (CUF)
Kura - 72,885

Philipo John Fumbo (DP)
Kura - 8,283

Membe Benard Kamillius(ACT)
Kura - 81,129

Queen Curthibert Sendiga (ADC)
Kura - 7627

Twalib Ibrahim Kadege (UPDP)
kura - 6194

Rungwe Hashim Spunda (CHAUMMA)
Kura - 32,878

Mazrui Alfan Mohamed (UMD)
Kura - 3721

Seif Maalim Seif (AAFP)
Kura - 4,635

Lissu Tundu Antiphas Mughwai (CHADEMA)
Kura - 1,933,271

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments