TUNDU LISSU ADAI BADO HAJAPOKEA WITO WA MALALAMIKO

Mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amesema kuwa hadi sasa bado hajapokea wito wala malalamiko yoyote kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kama taarifa ya tume hiyo ilivyoeleza hapo jana.

Lissu ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 30, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, na na kusisitiza kuwa kwa sababu hana wito wowote yeye ataendelea na ratiba zake za kampeni kama ilivyo kwenye ratiba.

Jana Septemba 29, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dkt. Wilson Mahera alitoa taarifa ya kuthibitisha kumuandikia barua ya wito Tundu Lissu, kufuatia tuhuma mbalimbali anazodaiwa kuzitoa kati ya Septemba 25 na 26 mjini Musoma



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments