RAIS MAGUFULI ATEUA MKURUGENZI MPYA WA TAWIRI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Eblate Ernest Mjingo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI).



Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Mjingo alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Tiba ya Wanyamapori na Huduma za Maabara wa TAWIRI, na anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Simon Mduma ambaye amestaafu.

Uteuzi wa Dkt. Mjingo unaanza leo tarehe 29 Septemba, 2020.


 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments