TANESCO: Wananchi Changamkieni Fursa Fursa Za Umeme Wa Kutosha Kujiletea Maendeleo Na Mwandishi Wetu, Nyakabindi

Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuwahimiza wananchi wote wakiwemo, wakulima, wafugaji na wavuvi kutumia fursa za uwepo wa umeme wa kutosha na wa uhakika ili kujiletea maendeleo.

Hayo yamesemwa Agosti 2, 2020 na Meneja wa TANESCO mkoa wa Simiyu, Eng. Khadija Abdallahmed kwenye banda la TANESCO katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
 
“Naomba kutoa wito kwa watanzania wote kwa ujumla wachangamkie hizi fursa za umeme na maendeleo ya kilimo, mifugo na uvuvi Tanzania nzima, umeme upo wa kutosha Tanzania nzima, TANESCO tupo tunaaangaza maisha.” Alisisitiza Eng. Khadija
 
Alisema TANESCO inashiriki maonyesho haya kwa vile wao ni wadau wakubwa wa shughuli za kilimo, mifugo pamoja na uvuvi na kwa huduma ya umeme itolewayo na shirika hilo ni sehemu ya kufanikisha maonesho hayo.
 
Aliwakaribisha wananchi wote wanaopata fursa ya kufika kwenye viwanja vya Nyakabindi yanakofanyika maonesho hayo kutembeela katika banda la TANESCO kwani watafaidika na kupata elimu kuhusu matumizi bora na sahihi ya umeme.
 
“Lakini wananchi watakaofika kwenye banda letu watakutana na mtaalamu mbobezi ambaye atawaeleza kuhusu mradi mkubwaj wa kimkakati wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme Julius Nyerere (JNHPP 2115) kwenye bonde la mto Rufiji.” Alisema.
 Eng.Mwanji Y Mhaka, Mhandisi mradi wa umeme wa maji Julius Nyerere (JNHPP-2115) akitoa maelezo kwa wananchi waliofika kwenye banda la TANESCO kwenye maonesho ya Nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi wilayani Bariadi mkoani Simiyu Agosti 2, 2020.
 Elimu kuhusu matumizi bora ya umeme ikitolewa na mtaalamu huyu wa TANESCO kwa wakazi wa mji wa Bariadi mkoani Simiyu waliofika katika banda la Shirika hilo
 Wahudumu wa TANESCO wakiwahudumia wananchi waliofika kwenye banda la shirika hilo katika maonesho ya Nanenane viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
 Wahudumu wa TANESCO wakiwahudumia wananchi waliofika kwenye banda la shirika hilo katika maonesho ya Nanenane viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
 Meneja wa TANESCO mkoa wa Simiyu, Eng. Khadija Abdallahmed(Watano kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na timu ya wafanyakazi wa TANESCO katika banda la shirika hilo 
Wakubwa kwa watoto wakielimishwa kuhusu madhara yanayoweza kutokea endapo mtu atashika waya wa umeme uliokatika 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments