Ndege ya Shirika la Air India yaanguka uwanja wa ndege wa Calicut nchini India

Ndege ya Shirika la Air India iliyokuwa na abiria karibu 200 imeanguka katika uwanja wa ndege wa Calicut .

Ndege hiyo iliyokuwa ikitoka Dubai, ilianguka wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa jimbo la Kusini mwa India, Kerala.

Shughuli za uokoaji zinaendelea, huku huduma za dharura zikiwa zinaendelea uwanjani hapo.

Bado haijafahamika kama kuna madhara yoyote yaliyotokea. Picha zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zimeonesha ndege hiyo iliwa imevunjika vipande viwili.

Tukio hilo limetokea mwendo wa saa moja kwa saa za eneo hilo kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha

Kumekuwepo na mafuriko na maporomoko ya udongo, wakati huu wa kipindi cha monsoon.

Credit:BBC


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments