GGML YATHIBITISHA AHADI YAKE KUENDELEZA JAMII YA GEITA


Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Richard Jordinson (kulia) akikabidhi mkataba wa makubaliano Mpango wa uwajibika kwa jamii mwaka huu (CSR) kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (kushoto).
Baadhi ya maofisa kutoka kampuni ya GGML na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita wakisaini makubaliano hayo huku wakishuhudiwa na baadhi ya maofisa wengine.
Mkurugenzi wa Mji wa Geita, Mhandisi Modest Apolinary (kulia) na Mkurugenzi wa Wilaya ya Geita, Alli Kidwaka (kushoto) wakisaini makubaliano hayo.
Mkuu wa Sheria kutoka Kampuni ya AngloGold Ashanti - Geita Gold Mining Limited (GGML), David Nzaligo na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Richard Jordinson wakisaini makubaliano hayo.
****

NA MWANDISHI WETU
Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) pamoja na Halmashauri ya Mji wa Geita mapema jana imesaini makubaliano ya utekelezaji wa Mpango wa kusaidia Jamii (CSR) kwa mwaka 2020 wenye thamani ya Sh bilioni 9.2. 

Makubaliano hayo yamethibitisha ahadi GGML kwa Serikali baada ya kutekeleza mabadiliko yaliyomo kwenye kifungu cha 105 cha Sheria ya Madini ambacho kinajumuisha utekelezaji wa Mpango wa uwajibikaji kwa jamii (CSR).

Utekelezaji wa mpango huo wa CSR utanufaisha jamii ya Geita katika maeneo ya mazingira, miundombinu, afya, elimu na biashara ndogo na za kati (SMEs).

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini makubaliano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel alielezea namna Serikali ya inavyothamini ushirikiano mzuri uliopo kati GGML na jamii ya Geita.

Alisema GGML inajitahidi kusaidia Serikali za kuwa na maendeleo endelevu ya jamii na uchumi katika jamii ya mji wa Geita. 

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Richard Jordinson alisema hatua hiyo inatekeleza malengo ya kampuni hiyo kuendeleza ushirikiano na serikali za mitaa na jamii nzima kwa ujumla katika kutambua na kusimamia miradi muhimu kwa mustakabali endelevu wa mkoa wa Geita.

"Tunafurahi sana kuendeleza ahadi yetu kwa Serikali na jamii wenyeji. Katika mwaka huu wa tatu wa utekelezaji wa npanngo huu baada ya mabadiliko ya sheria ya madini, ni matumaini yetu kuwa tunaweza kuendeleza tulipoishia katika miradi iliyopita ili kuongeza tija na umiliki kwa jamii lakini pia kuendelea kuahidi ushirikiano katika miradi endelevu ambayo itaendelea kuwepo hata baada ya shughuli za mgodi.

“Tangu GGML ianzishwe, imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na serikali ya mkoa wa Geita kusaidia miradi kadhaa ya kijamii katika mkoa wa Geita kupitia ushirikiano baina ya Serikali na sekta binafsi (PPP) sanjari na mpango ya Kitaifa.

“Pamoja na tunu yake kuu ya kusaidia jamii ya Geita kuwa na maendeleo endelevu kijamii na kiuchumi ambayo yatabakia hata baada ya shughuli za uchimbaji kumalizika, pia kampuni imefadhili utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwamo usambazaji wa maji safi, uendelezaji wa shughuli za uchumi katika sekta za kilimo, ujenzi na huduma,” alisema. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527