TRUMP AVAA BARAKOA HADHARANI KWA MARA YA KWANZA


Rais Donald Trump wa Marekani hapo jana alivaa barakoa hadharani kwa mara ya kwanza ikiwa ni ishara ya kusalimu amri kwa shinikizo la kumtaka kuwa mfano kwa umma katika wakati janga la virusi vya corona linaendelea kuitikisa Marekani. 

Trump alionekana akiwa amefunika pua na mdomo kwa kutumia barakoa yenye nembo ya rais alipotembea hospitali moja ya kijeshi nje kidogo ya mji mkuu Washington alipokwenda kukutana na maveterani waliojeruhiwa. 

Duru zimearifu kuwa mapema wiki hii wasaidizi wake walimuomba kiongozi huyo kuvaa barakoa hadharani katika kipindi ambacho visa vya virusi vya corona vinaongezeka katika baadhi ya majimbo nchini Marekani.

 Trump ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa sharti la kuvaa barakoa, mara kadhaa ametetea jinsi utawala wake unavyolishughulikia suala la corona licha ya kwamba Marekani ndiyo taifa linaloongoza duniani kwa maambukizi pamoja na vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Covid-19. 

Credit:DW


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527