CHAMA CHA WAIGIZAJI WA FILAMU NA MICHEZO YA KUIGIZA TANZANIA CHATOA POLE KUFUATIA KIFO CHA RAIS MSTAAWAMU BENJAMIN MKAPA

( TDFAA - Tanzania Drama & Film Actors Association ).

Salamu Za Pole.

Sisi Chama Cha Waigizaji Nchini , Tumepokea Kwa Mshtuko na Masikitiko Makubwa Kifo Cha Mzee Wetu na Kipenzi Chetu Rais Mstaafu wa Awamu Ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa Kilichotokea Usiku Wa Kuamkia Leo 24,July,2020 Jijini Dar es salaam.

Chama Kinatoa Pole Kwa Mh. Rais Doctor John Pombe Magufuli , Chama Cha Mapinduzi , Familia Ya Mzee Mkapa na Watanzania Wote Kwa Ujumla , Tumempoteza Mmoja Kati Ya Watu ambao Tulitegemea Busara Zao Katika Kila Magumu Tunayopitia Kama Taifa .. Tutaendelea Kumkumbuka Kwa Juhudi na Uchapakazi Wake Kipindi alipokuwa Kiongozi Mkuu Wa Nchi Kwa Mipango Yake Mbali Mbali Iliyoonyesha anauchukia Umasikini wa Watanzania Kutoka Moyoni Kwa Kuanzisha MKUKUTA , MKURABITA na Miradi Mingineyo ambayo Kabla Yake Haiukuwahi Kuwepo.



Pumzika Kwa Amani Mzee Wetu Benjamin William Mkapa , Tulikupenda Ila Mungu amekuoenda Zaidi.

Taifa Litaendelea Kukukumbuka na Kukulilia DA I'm a.

 BWANA AMETOA , BWANA AMETWAA , JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Massoud Kaftany.
Afisa Habari , Uenezi na Mahusiano na Umma
Mawasiliano - +255 655 660 377


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527