BENARD MEMBE AREJESHA FOMU YA KUGOMBEA URAIS KUPITIA ACT WAZALENDO

Aliyewahi kuwa waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, leo Julai 19, 2020 amerejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo.



Makabidhiano hayo yamefanyika Ofisi ya ACT Wazalendo Magomeni, jijini Dar es salaam ambapo amekabidhi fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa ACT Wazalendo Ndugu Joran Bashange.

Membe ambaye kauli mbiu yake alitaja kuwa ni Kazi na Bata, alikubali kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo, kwa kile alichodai kwamba huo ni wakati muafaka kwake wa kushiriki mazungumzo na vyama vingine ili waweze kusimamisha mgombea mmoja.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527