RAIS MAGUFULI AAHIRISHA SHEREHE ZA MASHUJAA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli.

Rais Magufuli ameahirisha sherehe za mashujaa zilizopaswa kufanyika Julai 25, 2020, Jijini Dodoma na kuwataka Watanzania kuitumia siku hiyo kuwakumbuka na kuwaombea mashujaa wote waliojitoa kwa ajili ya Tanzania.

Taarifa hiyo imetolewa leo Julai 18, 2020, na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, na kuongeza kuwa Rais Magufuli amewataka Watanzania kuendelea kudumisha amani, upendo, utulivu na mshikamano.

Aidha Rais Magufuli pia amewataka Watanzania kuwaombea Mashujaa wote hata wale ambao wametoa mchango mkubwa katika ngazi mbalimbali, ikiwemo kwa mtu mmoja mmoja ama familia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527