NAIBU SPIKA DKT TULIA ACKSON AKIWASILI HOSPITALI KUMJULIA HALI FREEMAN MBOWE ALIYEVAMIWA NA KUVUNJWA MGUU DODOMA


Naibu Spika, Dkt Tulia Ackson akiwasili katika Hospitali ya DCMC Ntyuka kumjulia hali M/Kiti wa Chadema na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliyelazwa katika hospitali hiyo akipatiwa matibabu baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana.


*****

Naibu Spika, Dk.Tulia Ackson  amemjulia hali Mwenyekiti Chadema, Freeman Mbowe katika Hospitali ya Ntyuka, Dodoma anakopatiwa matibabu  baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana na kisha kujeruhiwa na kuvunjwa mguu mmoja na kusema kuwa amemuona akiwa na majeraha mguuni na kwamba wanasubiri taarifa ya daktari ili kujua ameumia kwa kiasi gani.

"Ana maumivu ya mguu, mimi nimemuona ila bado wanaendelea kufanya uchunguzi na vipimo vingine, niwatoe hofu watanzania kwamba yupo anaendelea kupata huduma"- Amesema Naibu Spika Baada ya kumtembelea Mbowe 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527