WAZIRI MKUU WA URUSI AKUTWA NA VIRUSI VYA CORONA


Waziri Mkuu wa Russia Mikhail Mishustin amesema amekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Serikali ya Urusi imesema, Mishustin alimwambia rais wa nchi hiyo Vladmir Putin kwa njia ya video kuwa, amepimwa na kukutwa na virusi vya Corona. 

Amesema amejitenga nyumbani kwake na kufuata maelekezo ya madaktari, na kuongeza kuwa, serikali itaendelea kufanya kazi kama kawaida.

Naibu wa kwanza wa Waziri Mkuu huyo Andrei Belousov atakaimu kwa muda kazi za waziri mkuu huyo, kufuatia hatua iliyoidhinishwa na rais Putin.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post