VIFO VYA CORONA MAREKANI VYAPINDUKIA 102,107


 Idadi ya wagonjwa waliofariki kutokana na virusi vya corona nchini Marekani imefika  102,107 katika kipindi cha chini ya miezi minne.

Taifa hilo limeandikisha vifo vingi zaidi ya taifa lolote lile huku watu 1,745,803  wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo idadi ambayo ni asilimia 30 ya maambukizi yote duniani.

Maambukizi ya kwanza nchini Marekani yaliripotiwa mjini Washington tarehe 21 mwezi Januari.

Kufikia sasa idadi ya waliofariki nchini Marekani imefikia 102,107, kulingana na Chuo kikuu cha John Hopkins mjini Maryland ,ambacho kimekuwa kikifuatilia mlipuko huo. Waliopona 490,130


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527