MSHUMAA WAUNGUZA NYUMBA NA KUUA WATOTO


Watoto wawili wamefariki Dunia kufuatia kuungua moto kwa nyumba waliyokuwa wakiishi, katika mtaa wa Makuburi Ubungo jijini Dar es salaam. 

Akizungumza na EA Radio Mwenyekiti wa Mtaa Makuburi, Moshi Kaftany amesema chanzo cha moto inadaiwa ni mshumaa.

Kaftany amesema kuwa "moto umetokea usiku wa kuamkia leo na wajukuu zangu wawili wamefariki, bahati mbaya zaidi, hakuna hata mpangaji aliyefanikiwa kuokoa chochote"

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post