WANAODAIWA KUWA MAJAMBAZI WAVAMIA NA KUPORA MATAIRI YA GARI LA KAMANDA WA POLISI GEITA


Jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia watu wawili waodaiwa kuwa ni majambazi huku likiendelea kuwasaka watu kadhaa kwa tuhuma za kuvamia usiku wa manane eneo lililokuwa limehifadhiwa gari la kamanda wa polisi mkoa huo na kuiba matairi yake yote manne kisha kutokomea pasipojulikana.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Mponjoli Lotson anasema katika hali isiyo ya kawaida watu hao kwa kushirikiana na walinzi walifanya uporaji huo kwa kufungua matairi hayo kisha kutokomea nayo huku jeshi hilo likiendelea na msako ili wahusika wote wakamatwe na kuchukuliwa hatua. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527