AKAMATWA KWA KUVAA SARE ZA JWTZ ALIZOIBA KWA BABA MKWE ILI ASILIPE NAULI KATIKA BASI



Jeshi la Polisi mkoani Kagera, linamshikilia Mrisho Ibrahimu mwenye umri wa miaka 34 kwa tuhuma za kukutwa na sare za Jeshi la Wananchi (JWTZ), ambazo imedaiwa aliziiba kutoka katika nyumba ya Baba Mkwe wake, mkoani Arusha.

Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe amesema, alichukua nguo hizo ili asilipe nauli katika basi.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kagera, Revocatus Malimi amesema kuwa kijana huyo alikamatwa akiwa katika nyumba moja ya kulala wageni, eneo la Kamachumu wilayani Muleba, na kuwa alipohojiwa amekiri kuiba sare za baba mkwe wake, ambaye ni Askari wa JWTZ mkoani Iringa, na kujifanya ni Askari wa Jeshi hilo kikosi cha mizinga mkoani Arusha.

Akieleza sababu ya kufika mkoani Kagera, Kijana Mrisho Ibrahimu amesema, alimfuata mpenzi wake wa kando (mchepuko) ambaye alimpata kupitia mitandao ya kijamii na kuwa alipofika mkoani humo hakubahatika kukutana naye, ndipo alipoanza kufanya utapeli ili apate nauli ya kurudi alipotoka

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527