RAIS MAGUFULI : BAADHI YA VIONGOZI WA DINI WAMEANZA KUYUMBA..WAMEMSAHAU MUNGU KWENYE CORONA



Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema baadhi ya viongozi wa dini wameanza kuyumba na kumsahau Mungu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.


 Rais Mafuguli ameyasema leo Jumapili Mei 3,2020 akiwa Chato Mkoani Geita wakati wa hafla fupi ya kumuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Malunde 1 blog imefuatilia hotuba ya Rais Magufuli iliyokuwa inarushwa Live katika vyombo vya na imefanikiwa kupata nukuu zifuatazo

⇒⇒⇒"Wapo hadi baadhi ya viongozi wa dini wamemsahau Mungu ambaye kila siku wamekuwa wakituhubiria, wanashika vitabu wanafahamu yupo Mungu" - Rais Magufuli.

⇒⇒⇒Leo kuna baadhi ya viongozi wa dini wameanza kuyumba na kumsahau Mungu ambaye waliapa ndiyo kiapo chao Biblia au Quraan,wameanza kuisahau na kuiweka pembeni na kuuweka ubinadamu mbele.. Acheni kuomba tunajiokoa,acheni sijui nini nini..

⇒⇒⇒Ni mambo ya ajabu lakini ndiyo hivyo katika kipindi hiki cha mpito tutayasikia mengi na huu ndiyo wakati wa kuwapima imani viongozi tulionao.. Hata viongozi wa dini ..ukizuia waumini wako wasiende kanisani,ukazuia waumini wako wasiende msikitini na unaweza ukakuta hata huo msikiti wala hukuujenga wewe,umejengwa na hao waumini..hilo nalo ni suala la ajabu la kujiuliza, si uwafungulie hao waumini wenye nia waende mle wakamuombe Mungu hata kama wewe hutaenda kuhubiri pale?

⇒⇒⇒Ndiyo hapa tutayaona, na hizi ni changamoto..Tuendelee kumuomba Mungu na Mungu atatusaidia katika kutupitisha kwenye changamoto hizi wala hali siyo mbaya kama inavyotishwa sisi tupo vizuri na biashara zinaendelea na ndiyo maana tuna uwezo wa kulipa hata mishahara" - JPM

⇒⇒⇒Tufunge kila kitu utawalipa mishahara? hata wanaozungumza hao funga huku wanaendesha magari yameandika STK,mafuta yanawekwa mule na serikali lakini anasema fungeni,amesahau alichokalia ndiyo kinachomlisha..

⇒⇒⇒Watanzania simameni Imara,huu ugonjwa utaisha,utapita tunapata changamoto lakini tunazitatua.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post