RAIS MAGUFULI AWAONYA VIJANA WANAOPOST UJINGA KUHUSU CORONA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Watanzania kubadilika na kuacha tabia ya kuichafua nchi na kuogopesha wananchi kuhusu ugonjwa wa Corona kwamba kila mtu anayekufa basi ameugua Corona.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jumapili Mei 3,2020 wakati akiwa Chato mkoani Geita akimuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

"Corona kweli ipo lakini isituyumbishe katika msimamo wetu na direction yetu , Tusitishwe',amesema Rais Magufuli.

 "Naendelea kutoa wito kwa hasa vijana ambao wamekuwa kila siku wanapost, wakimuona mtu, amekufa na Corona..Marehemu Jaji Mkuu tumehangaika naye zaidi ya mwaka mzima, siyo vizuri kutaja matatizo yake..Jaji Mkuu amekufa kwa Kansa lakini watu wamebadilisha maneno ya ajabu",amesema Rais Magufuli.

"Kwa hiyo Watanzania tujifunze hata kumuogopa Mungu,Tujifunze hata kumuogopa mtu, si vyema kila mtu anayekufa ni Corona..It is not Possible..Mbona Maleria yameua watu wengi tu,mbona ajali zimeua watu wengi tu.

"Siku hizi hata mtu akikutwa na ajali polisi wanakwenda,wanavaa gloves zao wanasema huyu ana Corona,mtu hata akijiua chumbani kwake wanapokwenda kuchukua mwili wake wanasema ni Corona..Ninawaomba Watanzania tubadilike, Tunaichafua nchi yetu,tunaiharibu nchi yetu,tunajiogopesha sisi wenyewe wakati hili suala Mungu atali - Handle na tutapita salama",amesema JPM

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post